94:3Ulio vunja mgongo wako?
94:4Na tukakunyanyulia utajo wako?
94:5Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
94:6Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
94:7Na ukipata faragha, fanya juhudi.
94:8Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
95:1Naapa kwa tini na zaituni!
95:2Na kwa Mlima wa Sinai!
95:3Na kwa mji huu wenye amani!
95:4Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
95:5Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
95:6Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
95:7Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
95:8Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?
96:1Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
96:2Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
96:3Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
96:4Ambaye amefundisha kwa kalamu.
96:5Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
96:6Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
96:7Akijiona katajirika.
96:8Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
96:9Umemwona yule anaye mkataza
96:10Mja anapo sali?
96:11Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
96:12Au anaamrisha uchamngu?