Inapakia...
112:1Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
112:2Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
112:3Hakuzaa wala hakuzaliwa.
112:4Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.
113:1Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,
113:2Na shari ya alivyo viumba,
113:3Na shari ya giza la usiku liingiapo,
113:4Na shari ya wanao pulizia mafundoni,
113:5Na shari ya hasidi anapo husudu.
114:1Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa wanaadamu,
114:2Mfalme wa wanaadamu,
114:3Mungu wa wanaadamu,
114:4Na shari ya wasiwasi wa Shetani, Khannas,
114:5Anaye tia wasiwasi katika vifua vya watu,
114:6Kutokana na majini na wanaadamu.