Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/49

الطور

At-Tur

Tûr

Makkiyya·Aya 49

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

52:1
Juz 27
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

وَٱلطُّورِ﴿١﴾

Naapa kwa mlima wa T'ur,

—
52:2
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

وَكِتَـٰبٍ مَّسْطُورٍ﴿٢﴾

Na Kitabu kilicho andikwa

—
52:3
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

فِى رَقٍّ مَّنشُورٍ﴿٣﴾

Katika ngozi iliyo kunjuliwa,

—
52:4
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

وَٱلْبَيْتِ ٱلْمَعْمُورِ﴿٤﴾

Na kwa Nyumba iliyo jengwa,

—
52:5
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

وَٱلسَّقْفِ ٱلْمَرْفُوعِ﴿٥﴾

Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,

—
52:6
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

وَٱلْبَحْرِ ٱلْمَسْجُورِ﴿٦﴾

Na kwa bahari iliyo jazwa,

—
52:7
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٌ﴿٧﴾

Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.

—
52:8
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٍ﴿٨﴾

Hapana wa kuizuia.

—
52:9
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

يَوْمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوْرًا﴿٩﴾

Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,

—
52:10
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

وَتَسِيرُ ٱلْجِبَالُ سَيْرًا﴿١٠﴾

Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.

—
52:11
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

فَوَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ﴿١١﴾

Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,

—
52:12
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

ٱلَّذِينَ هُمْ فِى خَوْضٍ يَلْعَبُونَ﴿١٢﴾

Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.

—
52:13
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا﴿١٣﴾

Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,

—
52:14
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 523

هَـٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِى كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ﴿١٤﴾

(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!

—
52:15
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

أَفَسِحْرٌ هَـٰذَآ أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ﴿١٥﴾

Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?

—
52:16
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

ٱصْلَوْهَا فَٱصْبِرُوٓا۟ أَوْ لَا تَصْبِرُوا۟ سَوَآءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿١٦﴾

Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.

—
52:17
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

إِنَّ ٱلْمُتَّقِينَ فِى جَنَّـٰتٍ وَنَعِيمٍ﴿١٧﴾

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,

—
52:18
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

فَـٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَىٰهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ ٱلْجَحِيمِ﴿١٨﴾

Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.

—
52:19
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

كُلُوا۟ وَٱشْرَبُوا۟ هَنِيٓـًٔۢا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿١٩﴾

Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.

—
52:20
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَّصْفُوفَةٍ ۖ وَزَوَّجْنَـٰهُم بِحُورٍ عِينٍ﴿٢٠﴾

Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.

—
52:21
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَٱتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَـٰنٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَآ أَلَتْنَـٰهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَىْءٍ ۚ كُلُّ ٱمْرِئٍۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ﴿٢١﴾

Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.

—
52:22
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

وَأَمْدَدْنَـٰهُم بِفَـٰكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ﴿٢٢﴾

Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.

—
52:23
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

يَتَنَـٰزَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَّا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ﴿٢٣﴾

Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.

—
52:24
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

۞ وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَّكْنُونٌ﴿٢٤﴾

Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.

—
52:25
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَآءَلُونَ﴿٢٥﴾

Wataelekeana wakiulizana.

—
52:26
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

قَالُوٓا۟ إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِىٓ أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ﴿٢٦﴾

Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;

—
52:27
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ﴿٢٧﴾

Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.

—
52:28
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلْبَرُّ ٱلرَّحِيمُ﴿٢٨﴾

Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.

—
52:29
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

فَذَكِّرْ فَمَآ أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ﴿٢٩﴾

Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.

—
52:30
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيْبَ ٱلْمَنُونِ﴿٣٠﴾

Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.

—
52:31
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 524

قُلْ تَرَبَّصُوا۟ فَإِنِّى مَعَكُم مِّنَ ٱلْمُتَرَبِّصِينَ﴿٣١﴾

Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.

—
52:32
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَـٰمُهُم بِهَـٰذَآ ۚ أَمْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ﴿٣٢﴾

Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?

—
52:33
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥ ۚ بَل لَّا يُؤْمِنُونَ﴿٣٣﴾

Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!

—
52:34
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

فَلْيَأْتُوا۟ بِحَدِيثٍ مِّثْلِهِۦٓ إِن كَانُوا۟ صَـٰدِقِينَ﴿٣٤﴾

Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.

—
52:35
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ خُلِقُوا۟ مِنْ غَيْرِ شَىْءٍ أَمْ هُمُ ٱلْخَـٰلِقُونَ﴿٣٥﴾

Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

—
52:36
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ خَلَقُوا۟ ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَٱلْأَرْضَ ۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ﴿٣٦﴾

Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.

—
52:37
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ عِندَهُمْ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ ٱلْمُصَۣيْطِرُونَ﴿٣٧﴾

Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

—
52:38
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ ۖ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُم بِسُلْطَـٰنٍ مُّبِينٍ﴿٣٨﴾

Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!

—
52:39
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ لَهُ ٱلْبَنَـٰتُ وَلَكُمُ ٱلْبَنُونَ﴿٣٩﴾

Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?

—
52:40
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ تَسْـَٔلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ﴿٤٠﴾

Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?

—
52:41
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ عِندَهُمُ ٱلْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ﴿٤١﴾

Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?

—
52:42
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًا ۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُوا۟ هُمُ ٱلْمَكِيدُونَ﴿٤٢﴾

Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.

—
52:43
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

أَمْ لَهُمْ إِلَـٰهٌ غَيْرُ ٱللَّهِ ۚ سُبْحَـٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٤٣﴾

Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.

—
52:44
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

وَإِن يَرَوْا۟ كِسْفًا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطًا يَقُولُوا۟ سَحَابٌ مَّرْكُومٌ﴿٤٤﴾

Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.

—
52:45
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَـٰقُوا۟ يَوْمَهُمُ ٱلَّذِى فِيهِ يُصْعَقُونَ﴿٤٥﴾

Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.

—
52:46
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

يَوْمَ لَا يُغْنِى عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْـًٔا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ﴿٤٦﴾

Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.

—
52:47
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا۟ عَذَابًا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ﴿٤٧﴾

Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.

—
52:48
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

وَٱصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا ۖ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ﴿٤٨﴾

Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,

—
52:49
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 525

وَمِنَ ٱلَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَـٰرَ ٱلنُّجُومِ﴿٤٩﴾

Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.

—
Aya IliyotanguliaAdh-DhariyatAya InayofuataAn-Najm