68:43Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
68:44Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
68:45Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
68:46Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
68:47Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
68:48Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
68:49Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
68:50Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
68:51Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
68:52Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
69:1Tukio la haki.
69:2Nini hilo Tukio la haki?
69:3Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
69:4Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
69:5Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
69:6Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
69:7Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
69:8Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?