Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/62

النجم

An-Najm

Necm

Makkiyya·Aya 62

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

53:1
Juz 27
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

وَٱلنَّجْمِ إِذَا هَوَىٰ﴿١﴾

Naapa kwa nyota inapo tua,

—
53:2
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمْ وَمَا غَوَىٰ﴿٢﴾

Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.

—
53:3
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلْهَوَىٰٓ﴿٣﴾

Wala hatamki kwa matamanio.

—
53:4
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْىٌ يُوحَىٰ﴿٤﴾

Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;

—
53:5
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلْقُوَىٰ﴿٥﴾

Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,

—
53:6
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

ذُو مِرَّةٍ فَٱسْتَوَىٰ﴿٦﴾

Mwenye kutua, akatulia,

—
53:7
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

وَهُوَ بِٱلْأُفُقِ ٱلْأَعْلَىٰ﴿٧﴾

Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.

—
53:8
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ﴿٨﴾

Kisha akakaribia na akateremka.

—
53:9
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

فَكَانَ قَابَ قَوْسَيْنِ أَوْ أَدْنَىٰ﴿٩﴾

Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.

—
53:10
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

فَأَوْحَىٰٓ إِلَىٰ عَبْدِهِۦ مَآ أَوْحَىٰ﴿١٠﴾

Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.

—
53:11
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

مَا كَذَبَ ٱلْفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ﴿١١﴾

Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.

—
53:12
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

أَفَتُمَـٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ﴿١٢﴾

Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?

—
53:13
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

وَلَقَدْ رَءَاهُ نَزْلَةً أُخْرَىٰ﴿١٣﴾

Na akamwona mara nyingine,

—
53:14
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

عِندَ سِدْرَةِ ٱلْمُنتَهَىٰ﴿١٤﴾

Penye Mkunazi wa mwisho.

—
53:15
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلْمَأْوَىٰٓ﴿١٥﴾

Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.

—
53:16
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

إِذْ يَغْشَى ٱلسِّدْرَةَ مَا يَغْشَىٰ﴿١٦﴾

Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.

—
53:17
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

مَا زَاغَ ٱلْبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ﴿١٧﴾

Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.

—
53:18
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

لَقَدْ رَأَىٰ مِنْ ءَايَـٰتِ رَبِّهِ ٱلْكُبْرَىٰٓ﴿١٨﴾

Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.

—
53:19
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

أَفَرَءَيْتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلْعُزَّىٰ﴿١٩﴾

Je! Mmemuona Lata na Uzza?

—
53:20
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلْأُخْرَىٰٓ﴿٢٠﴾

Na Manaat, mwingine wa tatu?

—
53:21
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلْأُنثَىٰ﴿٢١﴾

Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?

—
53:22
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

تِلْكَ إِذًا قِسْمَةٌ ضِيزَىٰٓ﴿٢٢﴾

Huo ni mgawanyo wa dhulma!

—
53:23
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

إِنْ هِىَ إِلَّآ أَسْمَآءٌ سَمَّيْتُمُوهَآ أَنتُمْ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلْطَـٰنٍ ۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهْوَى ٱلْأَنفُسُ ۖ وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلْهُدَىٰٓ﴿٢٣﴾

Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.

—
53:24
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

أَمْ لِلْإِنسَـٰنِ مَا تَمَنَّىٰ﴿٢٤﴾

Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?

—
53:25
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

فَلِلَّهِ ٱلْـَٔاخِرَةُ وَٱلْأُولَىٰ﴿٢٥﴾

Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.

—
53:26
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 526

۞ وَكَم مِّن مَّلَكٍ فِى ٱلسَّمَـٰوَٰتِ لَا تُغْنِى شَفَـٰعَتُهُمْ شَيْـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعْدِ أَن يَأْذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرْضَىٰٓ﴿٢٦﴾

Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.

—
53:27
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِٱلْـَٔاخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلْمَلَـٰٓئِكَةَ تَسْمِيَةَ ٱلْأُنثَىٰ﴿٢٧﴾

Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.

—
53:28
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنْ عِلْمٍ ۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ ۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغْنِى مِنَ ٱلْحَقِّ شَيْـًٔا﴿٢٨﴾

Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.

—
53:29
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

فَأَعْرِضْ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكْرِنَا وَلَمْ يُرِدْ إِلَّا ٱلْحَيَوٰةَ ٱلدُّنْيَا﴿٢٩﴾

Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.

—
53:30
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

ذَٰلِكَ مَبْلَغُهُم مِّنَ ٱلْعِلْمِ ۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ ٱهْتَدَىٰ﴿٣٠﴾

Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.

—
53:31
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَلِلَّهِ مَا فِى ٱلسَّمَـٰوَٰتِ وَمَا فِى ٱلْأَرْضِ لِيَجْزِىَ ٱلَّذِينَ أَسَـٰٓـُٔوا۟ بِمَا عَمِلُوا۟ وَيَجْزِىَ ٱلَّذِينَ أَحْسَنُوا۟ بِٱلْحُسْنَى﴿٣١﴾

Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.

—
53:32
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

ٱلَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَـٰٓئِرَ ٱلْإِثْمِ وَٱلْفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَ ۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلْمَغْفِرَةِ ۚ هُوَ أَعْلَمُ بِكُمْ إِذْ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلْأَرْضِ وَإِذْ أَنتُمْ أَجِنَّةٌ فِى بُطُونِ أُمَّهَـٰتِكُمْ ۖ فَلَا تُزَكُّوٓا۟ أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ﴿٣٢﴾

Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.

—
53:33
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

أَفَرَءَيْتَ ٱلَّذِى تَوَلَّىٰ﴿٣٣﴾

Je! Umemwona yule aliye geuka?

—
53:34
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَأَعْطَىٰ قَلِيلًا وَأَكْدَىٰٓ﴿٣٤﴾

Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?

—
53:35
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

أَعِندَهُۥ عِلْمُ ٱلْغَيْبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ﴿٣٥﴾

Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?

—
53:36
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

أَمْ لَمْ يُنَبَّأْ بِمَا فِى صُحُفِ مُوسَىٰ﴿٣٦﴾

Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?

—
53:37
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَإِبْرَٰهِيمَ ٱلَّذِى وَفَّىٰٓ﴿٣٧﴾

Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?

—
53:38
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ﴿٣٨﴾

Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?

—
53:39
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَـٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ﴿٣٩﴾

Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?

—
53:40
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَأَنَّ سَعْيَهُۥ سَوْفَ يُرَىٰ﴿٤٠﴾

Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?

—
53:41
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

ثُمَّ يُجْزَىٰهُ ٱلْجَزَآءَ ٱلْأَوْفَىٰ﴿٤١﴾

Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.

—
53:42
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلْمُنتَهَىٰ﴿٤٢﴾

Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.

—
53:43
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضْحَكَ وَأَبْكَىٰ﴿٤٣﴾

Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.

—
53:44
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 527

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحْيَا﴿٤٤﴾

Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.

—
53:45
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوْجَيْنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلْأُنثَىٰ﴿٤٥﴾

Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike

—
53:46
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

مِن نُّطْفَةٍ إِذَا تُمْنَىٰ﴿٤٦﴾

Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.

—
53:47
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَأَنَّ عَلَيْهِ ٱلنَّشْأَةَ ٱلْأُخْرَىٰ﴿٤٧﴾

Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.

—
53:48
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغْنَىٰ وَأَقْنَىٰ﴿٤٨﴾

Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.

—
53:49
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعْرَىٰ﴿٤٩﴾

Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.

—
53:50
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَأَنَّهُۥٓ أَهْلَكَ عَادًا ٱلْأُولَىٰ﴿٥٠﴾

Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,

—
Aya IliyotanguliaAt-TurAya InayofuataAl-Qamar