Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/55

القمر

Al-Qamar

Kamer

Makkiyya·Aya 55

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

54:1
Juz 27
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

ٱقْتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلْقَمَرُ﴿١﴾

Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!

—
54:2
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَإِن يَرَوْا۟ ءَايَةً يُعْرِضُوا۟ وَيَقُولُوا۟ سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ﴿٢﴾

Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.

—
54:3
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَكَذَّبُوا۟ وَٱتَّبَعُوٓا۟ أَهْوَآءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ﴿٣﴾

Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.

—
54:4
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

وَلَقَدْ جَآءَهُم مِّنَ ٱلْأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ﴿٤﴾

Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.

—
54:5
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

حِكْمَةٌۢ بَـٰلِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ ٱلنُّذُرُ﴿٥﴾

Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!

—
54:6
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 528

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَىْءٍ نُّكُرٍ﴿٦﴾

Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;

—
54:7
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

خُشَّعًا أَبْصَـٰرُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ ٱلْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ﴿٧﴾

Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,

—
54:8
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

مُّهْطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِ ۖ يَقُولُ ٱلْكَـٰفِرُونَ هَـٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ﴿٨﴾

Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.

—
54:9
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

۞ كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا۟ عَبْدَنَا وَقَالُوا۟ مَجْنُونٌ وَٱزْدُجِرَ﴿٩﴾

Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.

—
54:10
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّى مَغْلُوبٌ فَٱنتَصِرْ﴿١٠﴾

Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!

—
54:11
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

فَفَتَحْنَآ أَبْوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٍ مُّنْهَمِرٍ﴿١١﴾

Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.

—
54:12
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

وَفَجَّرْنَا ٱلْأَرْضَ عُيُونًا فَٱلْتَقَى ٱلْمَآءُ عَلَىٰٓ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ﴿١٢﴾

Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.

—
54:13
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

وَحَمَلْنَـٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَٰحٍ وَدُسُرٍ﴿١٣﴾

Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.

—
54:14
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

تَجْرِى بِأَعْيُنِنَا جَزَآءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ﴿١٤﴾

Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.

—
54:15
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

وَلَقَد تَّرَكْنَـٰهَآ ءَايَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ﴿١٥﴾

Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?

—
54:16
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ﴿١٦﴾

Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.

—
54:17
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ﴿١٧﴾

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?

—
54:18
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ﴿١٨﴾

Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

—
54:19
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِى يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ﴿١٩﴾

Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,

—
54:20
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ﴿٢٠﴾

Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.

—
54:21
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ﴿٢١﴾

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?

—
54:22
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ﴿٢٢﴾

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?

—
54:23
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ﴿٢٣﴾

Thamudi waliwakanusha Waonyaji.

—
54:24
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

فَقَالُوٓا۟ أَبَشَرًا مِّنَّا وَٰحِدًا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذًا لَّفِى ضَلَـٰلٍ وَسُعُرٍ﴿٢٤﴾

Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!

—
54:25
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

أَءُلْقِىَ ٱلذِّكْرُ عَلَيْهِ مِنۢ بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ﴿٢٥﴾

Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!

—
54:26
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ ٱلْكَذَّابُ ٱلْأَشِرُ﴿٢٦﴾

Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.

—
54:27
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 529

إِنَّا مُرْسِلُوا۟ ٱلنَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَٱرْتَقِبْهُمْ وَٱصْطَبِرْ﴿٢٧﴾

Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.

—
54:28
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ ٱلْمَآءَ قِسْمَةٌۢ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ﴿٢٨﴾

Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.

—
54:29
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

فَنَادَوْا۟ صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ﴿٢٩﴾

Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.

—
54:30
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِى وَنُذُرِ﴿٣٠﴾

Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!

—
54:31
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَٰحِدَةً فَكَانُوا۟ كَهَشِيمِ ٱلْمُحْتَظِرِ﴿٣١﴾

Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.

—
54:32
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ﴿٣٢﴾

Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?

—
54:33
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍۭ بِٱلنُّذُرِ﴿٣٣﴾

Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.

—
54:34
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

إِنَّآ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَـٰهُم بِسَحَرٍ﴿٣٤﴾

Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.

—
54:35
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِى مَن شَكَرَ﴿٣٥﴾

Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.

—
54:36
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا۟ بِٱلنُّذُرِ﴿٣٦﴾

Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.

—
54:37
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَلَقَدْ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِۦ فَطَمَسْنَآ أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ﴿٣٧﴾

Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!

—
54:38
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ﴿٣٨﴾

Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.

—
54:39
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

فَذُوقُوا۟ عَذَابِى وَنُذُرِ﴿٣٩﴾

Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!

—
54:40
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَلَقَدْ يَسَّرْنَا ٱلْقُرْءَانَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ﴿٤٠﴾

Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?

—
54:41
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

وَلَقَدْ جَآءَ ءَالَ فِرْعَوْنَ ٱلنُّذُرُ﴿٤١﴾

Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.

—
54:42
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

كَذَّبُوا۟ بِـَٔايَـٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَـٰهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ﴿٤٢﴾

Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.

—
54:43
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُو۟لَـٰٓئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَآءَةٌ فِى ٱلزُّبُرِ﴿٤٣﴾

Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?

—
54:44
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ﴿٤٤﴾

Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.

—
54:45
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

سَيُهْزَمُ ٱلْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ﴿٤٥﴾

Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.

—
54:46
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَٱلسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ﴿٤٦﴾

Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.

—
54:47
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

إِنَّ ٱلْمُجْرِمِينَ فِى ضَلَـٰلٍ وَسُعُرٍ﴿٤٧﴾

Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.

—
54:48
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِى ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا۟ مَسَّ سَقَرَ﴿٤٨﴾

Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!

—
54:49
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 530

إِنَّا كُلَّ شَىْءٍ خَلَقْنَـٰهُ بِقَدَرٍ﴿٤٩﴾

Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.

—
54:50
Juz 27 · Hizb 53 · Ukurasa 531

وَمَآ أَمْرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٌ كَلَمْحٍۭ بِٱلْبَصَرِ﴿٥٠﴾

Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.

—
Aya IliyotanguliaAn-NajmAya InayofuataAr-Rahman