Ruka hadi Maudhui
NurVerse
QuraniNyakati za SwalaKalendaHadithiDua
Ad
Ad
Ad
Ad
NurVerse

Soma Qurani, fuatilia nyakati za swala, fanya dua, na utajirisha maisha yako ya Kiislamu.

© 2026 NurVerse. Haki zote zimehifadhiwa.

Sakinisha ProgramuWasilianaSera ya FaraghaMasharti ya Matumizi
Orodha ya Sura
Mtazamo wa Mushaf
0/20

المزمل

Al-Muzzammil

Müzzemmil

Makkiyya·Aya 20

بِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ

73:1
Juz 29
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلْمُزَّمِّلُ﴿١﴾

Ewe uliye jifunika!

—
73:2
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

قُمِ ٱلَّيْلَ إِلَّا قَلِيلًا﴿٢﴾

Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!

—
73:3
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

نِّصْفَهُۥٓ أَوِ ٱنقُصْ مِنْهُ قَلِيلًا﴿٣﴾

Nusu yake, au ipunguze kidogo.

—
73:4
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

أَوْ زِدْ عَلَيْهِ وَرَتِّلِ ٱلْقُرْءَانَ تَرْتِيلًا﴿٤﴾

Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.

—
73:5
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

إِنَّا سَنُلْقِى عَلَيْكَ قَوْلًا ثَقِيلًا﴿٥﴾

Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.

—
73:6
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

إِنَّ نَاشِئَةَ ٱلَّيْلِ هِىَ أَشَدُّ وَطْـًٔا وَأَقْوَمُ قِيلًا﴿٦﴾

Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.

—
73:7
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

إِنَّ لَكَ فِى ٱلنَّهَارِ سَبْحًا طَوِيلًا﴿٧﴾

Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.

—
73:8
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

وَٱذْكُرِ ٱسْمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلْ إِلَيْهِ تَبْتِيلًا﴿٨﴾

Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.

—
73:9
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

رَّبُّ ٱلْمَشْرِقِ وَٱلْمَغْرِبِ لَآ إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ فَٱتَّخِذْهُ وَكِيلًا﴿٩﴾

Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.

—
73:10
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

وَٱصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَٱهْجُرْهُمْ هَجْرًا جَمِيلًا﴿١٠﴾

Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.

—
73:11
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

وَذَرْنِى وَٱلْمُكَذِّبِينَ أُو۟لِى ٱلنَّعْمَةِ وَمَهِّلْهُمْ قَلِيلًا﴿١١﴾

Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!

—
73:12
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

إِنَّ لَدَيْنَآ أَنكَالًا وَجَحِيمًا﴿١٢﴾

Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!

—
73:13
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

وَطَعَامًا ذَا غُصَّةٍ وَعَذَابًا أَلِيمًا﴿١٣﴾

Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.

—
73:14
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

يَوْمَ تَرْجُفُ ٱلْأَرْضُ وَٱلْجِبَالُ وَكَانَتِ ٱلْجِبَالُ كَثِيبًا مَّهِيلًا﴿١٤﴾

Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!

—
73:15
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

إِنَّآ أَرْسَلْنَآ إِلَيْكُمْ رَسُولًا شَـٰهِدًا عَلَيْكُمْ كَمَآ أَرْسَلْنَآ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ رَسُولًا﴿١٥﴾

Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.

—
73:16
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

فَعَصَىٰ فِرْعَوْنُ ٱلرَّسُولَ فَأَخَذْنَـٰهُ أَخْذًا وَبِيلًا﴿١٦﴾

Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.

—
73:17
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

فَكَيْفَ تَتَّقُونَ إِن كَفَرْتُمْ يَوْمًا يَجْعَلُ ٱلْوِلْدَٰنَ شِيبًا﴿١٧﴾

Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?

—
73:18
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

ٱلسَّمَآءُ مُنفَطِرٌۢ بِهِۦ ۚ كَانَ وَعْدُهُۥ مَفْعُولًا﴿١٨﴾

Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.

—
73:19
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 574

إِنَّ هَـٰذِهِۦ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلًا﴿١٩﴾

Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.

—
73:20
Juz 29 · Hizb 58 · Ukurasa 575

۞ إِنَّ رَبَّكَ يَعْلَمُ أَنَّكَ تَقُومُ أَدْنَىٰ مِن ثُلُثَىِ ٱلَّيْلِ وَنِصْفَهُۥ وَثُلُثَهُۥ وَطَآئِفَةٌ مِّنَ ٱلَّذِينَ مَعَكَ ۚ وَٱللَّهُ يُقَدِّرُ ٱلَّيْلَ وَٱلنَّهَارَ ۚ عَلِمَ أَن لَّن تُحْصُوهُ فَتَابَ عَلَيْكُمْ ۖ فَٱقْرَءُوا۟ مَا تَيَسَّرَ مِنَ ٱلْقُرْءَانِ ۚ عَلِمَ أَن سَيَكُونُ مِنكُم مَّرْضَىٰ ۙ وَءَاخَرُونَ يَضْرِبُونَ فِى ٱلْأَرْضِ يَبْتَغُونَ مِن فَضْلِ ٱللَّهِ ۙ وَءَاخَرُونَ يُقَـٰتِلُونَ فِى سَبِيلِ ٱللَّهِ ۖ فَٱقْرَءُوا۟ مَا تَيَسَّرَ مِنْهُ ۚ وَأَقِيمُوا۟ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُوا۟ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَقْرِضُوا۟ ٱللَّهَ قَرْضًا حَسَنًا ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا۟ لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ ٱللَّهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ وَٱسْتَغْفِرُوا۟ ٱللَّهَ ۖ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌۢ﴿٢٠﴾

Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.

—
Aya IliyotanguliaAl-JinnAya InayofuataAl-Muddaththir