82:1Mbingu itapo chanika,
82:2Na nyota zitapo tawanyika,
82:3Na bahari zitakapo pasuliwa,
82:4Na makaburi yatapo fukuliwa,
82:5Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
82:6Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
82:7Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
82:8Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
82:9Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
82:10Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
82:11Waandishi wenye hishima,
82:12Wanayajua mnayo yatenda.
82:13Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
82:14Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
82:15Wataingia humo Siku ya Malipo.
82:16Na hawatoacha kuwamo humo.
82:17Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
82:18Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
82:19Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
83:1Ole wao hao wapunjao!
83:2Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
83:3Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
83:4Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa