90:19Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
90:20Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
91:1Naapa kwa jua na mwangaza wake!
91:2Na kwa mwezi unapo lifuatia!
91:3Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
91:4Na kwa usiku unapo lifunika!
91:5Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
91:6Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
91:7Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
91:8Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
91:9Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
91:10Na hakika amekhasiri aliye iviza.
91:11Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
91:12Alipo simama mwovu wao mkubwa,
91:13Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
91:14Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
91:15Wala Yeye haogopi matokeo yake.
92:1Naapa kwa usiku unapo funika!
92:2Na mchana unapo dhihiri!
92:3Na kwa Aliye umba dume na jike!
92:4Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
92:5Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
92:6Na akaliwafiki lilio jema,
92:7Tutamsahilishia yawe mepesi.
92:8Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
92:9Na akakanusha lilio jema,