100:6Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
100:7Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
100:8Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
100:9Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
100:10Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
100:11Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
101:1Inayo gonga!
101:2Nini Inayo gonga?
101:3Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
101:4Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
101:5Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
101:6Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
101:7Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
101:8Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
101:9Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
101:10Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
101:11Ni Moto mkali!
102:1Kumekushughulisheni kutafuta wingi,
102:2Mpaka mje makaburini!
102:3Sivyo hivyo! Mtakuja jua!
102:4Tena sivyo hivyo! Mtakuja jua!
102:5Sivyo hivyo! Lau mngeli jua kwa ujuzi wa yakini,
102:6Basi bila ya shaka mtaiona Jahannamu!
102:7Tena, bila ya shaka, mtaiona kwa jicho la yakini.
102:8Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya neema.