العصرAl-'Asrبِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
وَٱلْعَصْرِ﴿١﴾إِنَّ ٱلْإِنسَـٰنَ لَفِى خُسْرٍ﴿٢﴾إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوا۟ وَعَمِلُوا۟ ٱلصَّـٰلِحَـٰتِ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلْحَقِّ وَتَوَاصَوْا۟ بِٱلصَّبْرِ﴿٣﴾
103:1Naapa kwa Zama!
103:2Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,
103:3Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri.
الهمزةAl-Humazahبِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ﴿١﴾ٱلَّذِى جَمَعَ مَالًا وَعَدَّدَهُۥ﴿٢﴾يَحْسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخْلَدَهُۥ﴿٣﴾كَلَّا ۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِى ٱلْحُطَمَةِ﴿٤﴾وَمَآ أَدْرَىٰكَ مَا ٱلْحُطَمَةُ﴿٥﴾نَارُ ٱللَّهِ ٱلْمُوقَدَةُ﴿٦﴾ٱلَّتِى تَطَّلِعُ عَلَى ٱلْأَفْـِٔدَةِ﴿٧﴾إِنَّهَا عَلَيْهِم مُّؤْصَدَةٌ﴿٨﴾فِى عَمَدٍ مُّمَدَّدَةٍۭ﴿٩﴾
104:1Ole wake kila safihi, msengenyaji!
104:2Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
104:3Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
104:4Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
104:5Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
104:6Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
104:7Ambao unapanda nyoyoni.
104:8Hakika huo utafungiwa nao
104:9Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
الفيلAl-Filبِسْمِ ٱللَّهِ ٱلرَّحْمَـٰنِ ٱلرَّحِيمِ
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصْحَـٰبِ ٱلْفِيلِ﴿١﴾أَلَمْ يَجْعَلْ كَيْدَهُمْ فِى تَضْلِيلٍ﴿٢﴾وَأَرْسَلَ عَلَيْهِمْ طَيْرًا أَبَابِيلَ﴿٣﴾تَرْمِيهِم بِحِجَارَةٍ مِّن سِجِّيلٍ﴿٤﴾فَجَعَلَهُمْ كَعَصْفٍ مَّأْكُولٍۭ﴿٥﴾
105:1Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?
105:2Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
105:3Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
105:4Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
105:5Akawafanya kama majani yaliyo liwa!